Subscribe:

Ads 468x60px

Wednesday, October 9, 2013

UMEAMUA KUWA MAMA ?

Leo ningependa kuongelea wazo la kuwa mama na unyonyeshaji wa mtoto,
Mpendwa bloger tumesikia watu wengi wakilalamika kuhusu unyonyeshaji pamoja na ulaji ili kupata maziwa mengi, ni vitu vinavyoleta changamoto sana hasa kwa wamama ambao ndio kwanza wanaanza kuwa wamama,
Watu wengi sasa wameamasika kuhusu unyonyeshaji, ila wengi wenapata tatizo ni namna gani wanaweza kupata maziwa mengi ili yamtosheleze mtoto na asitumie maziwa mengine. Ikiwa wewe ni mama ambaye unajua ni jinsi gani hebu  tusaidiane katika hili uwe huru kutoa mawazo yako.

Mimi ni mama binafsi nina mtoto ambaye mpaka sasa nina mnyonyesha maziwa yangu, ninachofanya ni kula vyakula vingi vya majimamji pamoja na kunywa maji maji mengi kisi cha lita 2 kwa siku.
Kwa kufanya hivyo imenisaidia sana maziwa ni mengi na yanamtosha mtoto, jopokuwa ninachangamoto moja ambayo ni jinsi mtoto anavyosumbuliwa na gas, colic,  ni tatizo ambalo lina wasumbua watoto wengi ila mara nyingi linakwisha mtoto anapofika miezi 3, ila wapo baadhi ya watoto wanakwenda mpaka miezi 7 mpaka 10, hapo pia unaweza kumsaidia mtoto kwa kumtoa hewa mara anapomaliza kunyonya na pia kumlaza kwa tumbo.

WAZO LA LEO,
Mama hebu mnyonyeshe mtoto wako usione haya kutoa nyonyo , kwani si jambo la aibu, pia ukiona vipi tumia kitambaa au kanga kijifunika kumnyonyesha mtoto, kumbuka ni bahati ya kipekee wewe kuwa mama na kuweza kumnyonyesha mtoto wako.
WAZO LA LEO

Leo napenda kuongea na akina mama wenzangu, kuhusu kunyonyesha, hebu akina mama wote mnaonyonyesha jisikieni fahari kunyonyesha watoto wenu, binafsi nimeona baadhi ya akina mama wakiwa na watoto wadogo hawapendi kunyonyesha wanawapatia maziwa mengine tofauti na ya mama, ukweli ni kwamba kuna faida nyingi sana ukimnyonyesha mtoto.

hivyo kama wewe ni mama hebu jisikie fahari kumnyonyesha mwanao.

Monday, July 15, 2013

WAZO LA LEO - BIASHARA IMANI?

Hivi unajua kuwa si kila mfanyabiashara ni mjasiliamali, kwani tumeshuhudua biashara nyingi zilizoanzishwa zikifungwa tu kwa sababu mwenye hiyo biashara amestaafu kazi au amefukuzwa kazi n.k

Swali linakuja kama hiyo biashara inajiendesha na umeichukulia mkopo kwa nini ifungwe mara unapostaafu au kufukuzwa kazi, hebu tuzichunguze biashara zetu ni kweli zinatuingiza kipato na faida au ni bora tu kujiona kuwa na wewe pia umefungua biashara, au ni bora tu umetoka nyumbani na kwenda dukani kwako kama wengine wanavyofanya.

Tusijidanganye kwa kuchukua mshara na kulijaza duka , wakati mahesabu yanaonyesha kuwa hujaongeza faida na mauzo yako yameshuka. Ni bora ukae chini uangalie ni kwa jinsi gani utaongeza mauzo na faida bila kuisaidia kuibusti kwa mshahara wako.

Sunday, July 14, 2013

NIMERUDI TENA

Haya tena wanandugu nimerudi tena, baada ya kutokuwa na wewe mpenzi wa blog hii kwa muda usiopungua kama miezi 9, Kwa kweli niliwakosa na ninahamu nanyi  ili tujulishane yale yanayotuzunguka katika maisha yetu ya kila siku.
 
Nianze kwa kuwaomba radhi wle niliowakwanza kutokuwa kwangu hewani labda hakuwa wanapata kitu cha kusoma kutoka humu mara waingiapo ndani ya blog hii kweli inaboa nakuomba radhi, lakini nakuomba sasa uendelee kuingia kwani nimerudi kikamilifu sasa.
 yapo mengi ya kujuzana lakini kwa leo ngoja niishie hapo.

Friday, October 12, 2012

JE WAJUA

Ukishaolewa kwenu ni kwenda kusalimia tu na si kulala.

Kuna baadhi ya makabila hapa kwetu Tanzania yanamila ambazo hazimruhusu binti kurudi kwao kulala mara akisha olewa, na yapo baadhi ya makabila ni ruhusa unaweza kwenda kwenu kulala hata kama umeolewa ila uwe umepewa ruhusa na mumeo.

Nimepata babati ya kusoma mstari kati kitabu kitakatifu biblia na kugundua kuwa  si sahihi kwenda kwenu kulala mara unapoolewa kumbe makabila hayo yako sahihi kabisa kwa uhondo zaidi hebu zama ndani ya biblia zaburi 45 mstari wa 10-11.

Ni kitu cha kawaida siku izi kuona mabint wengi wakishaolewa kuwaona wapo majumbani kwa wazazi wao kwa vigezo vya kwenda kusalimia, au kwnda kujifungua na mambo mengine madogomadogo,. Imefikia hatua hata mtu akikorofishana na mumewe kidogo solution mtu anapaki mabegi anakwenda kwao

Hebu wewe dada,mama, au bint kaa chini ujiulize, kama kweli ulikuwa tayari kuolewa . Hukatazwi kwenda kwenu ila si kwenda kulala na mji wako unamwachia nani. Nenda salimia kama kuna shida saidi na kisha urudi kwako.

Wednesday, October 10, 2012

WAJISIKIAJE KUWAMJAMZITO KWA UMRI WAKO MKUBWA

UJAUZITO KWA UMRI HUO?

Kwa siku izi utasikia watu wakisema, ukiwa na umri wa miaka 35 na zaidi si jambo zuri kufikiria kuwa na mtoto, hasa pale ikiwa ndio mara ya kwanza kwa wewe kupata ujauzito na kwa wale ambao wanaendele pia madaktari wanashauri si vizuri sana kubeba ujauzito katika umri kama huo.

Lakini hebu tuangalie kuna ukweli gani,

Ukweli kwa kitaalamu upo, lakini basi mbona tumeshuhudia ndugu jamaa na marfiki wakifanikiwa kupata watoto kwa umri zaidi ya huo naamanisha watu wameweza kupata watoto katika umri mpaka miaka 45.

Ukweli ni kwamba tupo wengi tunahitaji watoto, ila kwa kusoma vitabu mbalimbali, na ushauri mbalimbali zilizotolewa na madakitari kumewatia uoga wamama, wadada wengi kufikiria kupata watoto katika umri zao hizo kubwa walizo nazo.

Mchangia mada mmoja alisema, siku izi tuanaolewa tukiwa na umri mkubwa tofauti na pale zamani, sasa tunafanyaje, ukweli ni kwamba muda mwingi tulikuwa tunaangaika na jinsi ya kuboresha vipato vyetu, na hata hao waoaji huwa wanakuja kidogo umri umekwenda sasa tufanye nini?

Kuna mwandishai mmoja yeye alisema mwisho wa siku ni wewe mwenyewe, kama kwa umri wako huo unayo afya nzuri, unakula vizuri na unafanya mazoezi vizuri hakuna haja ya kutia hofu, wewe kama unahitaji mtoto endelea na mpango wako huo na wala usihofu.

Mama mwingine yeye alisema siku izi kwa umri wake ukiwa mjamzito, hatakiwa kwenda clinic mapema kwani bainafsi anaona ni jambo la aibu kupishana na mabinti wadogo sawa na watoto wake huko clinic.

Ukweli unabakia pale pale wewe unayemtafuta mtoto ndio unajua umuhimu wa hiyo mimba uliyo nayo kwa umri huo, usiruhusu watu wakuamulie, au wakuhukumu, kwani hawakujui na wala hawajui ni kwanini umepata ujauzito katika umri kama huo. Cha msingi wewe be yourself.

kama kuna mwanamke yeyeto ambaye anaumri wa mika 35 na zaidi na ni mjamzito , napenda kukutia moyo, kujitunza, kuangalia unakula nini na ukiweza fanya mazoezi kidogo kidogo ni muhimu sana na usione aibu. Don't listen to judges, Be Yourself

Monday, October 8, 2012

KABLA HUJAONDOSHA GARI HEBU IKAGUE

Zunguka gari yako ,

Hiki si kichekesho wala utani ni kweli kabisa, wewe mama ambaye unaendesha gari au wewe baba unayeendesha gari, ni vizuri kuizunguka gari yako kabla huajaondosha mahali ilipo.  Ni kama kuchukua taadhari ili kuepusha vifo ambavyo labda vingezuilika hasa kwa watoto wadogo.

Haikuwa dhamira yake lakini ilitokea kama bahati mbaya, akamkanyaga mtoto amabaye alikuwa nyuma ya gari bila muhusika kufahamu yaani kama laiti yule dereva angezuka ile gari kuangalia kama kuna mtu au kitu chochote karibu na gari angeweza kuepusha kifo hicho.

wanasema ni kazi ya mungu, lakini kunakitu tunaweza kufanya mimi, wewe na yule, hatujazoea sawa lakini tunaweza kukianzisha sasa, ukiwa umepaki gari yako mahali popote tuwe na mazoea angalau kulizunguka kuangali kama kuna kitu au mtu yeyete karibu na gari.  Pia kiusama maranyingi mahali tunapoegesha magari huwa kunakuwa na wazi kwa kulikagua na kulizunguka gari lako unaweza kuona kama gari yako iko salama haijanyofolewa taa au kitu chochote zaidi ya yote ndio hilo la kuangalia usama wa watoto wetu.


Sunday, September 30, 2012

MSAIDIZI WANGU MTU MZIMA


Msaidizi wangu ni mkubwa kuliko mimi ,


Wamama wenzangu nakuja kwenu na hoja hii nakomaje!!!!
Nina mama mtu mzima ambaye ananisaidia shughuli za hapa nyumbani sasa ni mwaka wa pili, watu wananisifu kuwa nimeweza kuishi naye muda mrefu kwani nikiwa kama bosi naonekana mdogo kuliko yeye kwani ana umbo kubwa na mungu kamjalia mashalaa.
Ukweli mpaka nimeona nifunguke humu ni kwamba nakuwa kama namuogopa ukweli ninamuogopa kwani kunabaadhi ya vitu nashidwa kumwambia ukizingatia kuwa mimi ndio mama mwenye nyumba. Sasa nimekuwa najiuliza nifanye nini ili niweze kurudisha umama wangu nyumbani kwangu.
Kabla sijawa na huyu dada nilikuwa na dada mwingine mdogo kiumri na pia alikuwa mdogo kiumbo tofauti na huyu niliye naye sasa. Ukweli nikilinganisha hapo awali nilikuwa naendana na dada huyu mdogo vizuri ikiwa kuelekezana hata akikosea niliweza kumgombeza kwamba mbona hapa hivi na pale vile. Sasa bwana kivumbi kipo hapa kwa huyu mtu mzima kwanza anajiona anajua na vilevile  akikosea kumwambia wewe nakomaje, naishia kufanya mwenyewe baadhi ya kazi zile ambazo huwa hazifanyi vizuri kwa kuhofia kumwambia pale anapokose.
Ukweli ni kwamba anafanya baadhi ya kazi vizuri, na baadhi anakosea ila kwa upande wake yeye anaona ni sawa, Kumuhitaji namuhitaji kwani sina mtu mwingine wa kunisaidia na vile unajua siku hizi kuwapata hawa akina dada ni kazi.
Nasikitika pale ninapoona nimekuwa dhaifu wa kumwambia anapokosea kwa vile namuogopa kwa vile yeye ni mkubwa na mimi ni mdogo, na pia naogopa akiondoka kwa sasa sina mtu mwingine na mimi ninafanya kazi za kuajiriwa. Najua wazi mimi ndio boss na ninamamlaka yote ila nashidwa kumkoromea. Nayeye naona ameshagundua udhaifu wangu huo ananiangalia tu nafikiri ananichora tu. Mume wangu ananishangaa na ameshawahi kuniambia mbona unamuogopa mfanyakazi wako kama amekushinda mwachishe kazi .
Marafiki zangu hawajui kero hii ya huyu dada, ila hawaishi kumsifia kuwa eeh msichana wako ni mchapa kazi kama nini, na wanataka wapate wamama watu wazimz kama mimi. Nisaidieni jamani nifanye nini?

Thursday, September 27, 2012

Extended Families/ Familia pana

Familia pana au Kubwa,

Familia kubwa hii inamaanisha kuwa na familia zaidi ya mama ,baba na watoto.
Familia nyingi za kiafrika zinaishi na zaidi ya baba,mama na watoto wanasema kwa lugha ya kigeni extended families, Mimi ni mmoja ya watu tulioishi maisha ya namna hiyo nilipokuwa mdogo na mpaka nimeolewa bado naishi hivyo. kwa kifupi maisha ya namna hiyo ni kwa sabababu za umaskini au kipato kidogo kwa baadhi ya familia zetu .

 wengi wetu tuliopitia maisha haya tulijua iko siku yataisha, lakini nimegundua ni vigumu sana kumaliza hali hii, ikiwa vipato vya wanafamilia havijaimarika ni vigumu sana hali ya namna hii kuisha. sasa tufanyeje ili kumaliza hali hii kwa kifupi Ukiwa kama baba au mama mwenye nyumba ndiye mwenye uamuzi wa kumaliza au kubadilisha hali hiyo hapo kwako.

Binafsi nimeshuhudia baadhi ya familia zikipata taabu kwa ajili ya kuwahudumia ndugu hawa, inapofikia hatua mgeni wa hapo nyumbani kwako unamkabidhi chumba cha watoto wako na wewe unaishia kujibana na watoto kwenye chumba kimoja ukihofia kumlaza yeye na watoto wako hii ni hali mbaya sana.

kwa jinsi maisha yalivyo sasa watu wengi wamekuwa na tabia ambazo hazitabiriki, kiasi zinatisha kwa wewe mzazi kumlaza mtoto wako na mgeni yeyote atayekuja hapo ndani ukihofia jambo lolote baya analoweza kumfanyia mtoto. Hali kama hizi  zimepelekea watu wengi kuviacha vyumba vya watoto wao na kuwaachia wageni ambao wamekuja hapo nyumbani kutumia vyumba ambavyo mahususi viliandaliwa kwa ajili ya watoto na kutumiwa na wageni. Na watoto kuendelea kuchangia vyumba na wazazi wao na wasijue ni lini wataweza kuvipata vyumba vyao.

Kwa kweli hali kama hii inarudisha nyuma maendeleo kwani ni ndoto ya kila mzazi kuishi kisasa zaidi namaanisha, kila mtoto kuwa na chumba chake,  lakini kwa wakio wengi bado ni ndoto kwa ajili ya ndugu na jamaa ambao wengi wao bado ni tegemezi kwa familia zao.

basi kama wewe ni mmoja wa wageni unaye ishi katika familia za aina hii hebu chukua hatua ya kutafuta ni namna gani utaweza kujitegemea na kuwapa fursa watoto na wanafamilia angalau baada ya miaka kadhaa ya kusota chumbani kwa baba na mama hatimaye warumie vyumba vyao.

Saturday, August 25, 2012

MASOI SUMAYAN KITCHEN PARTY

Haya tena palikuwa hapatoshi kwa mama Victoria Sumayan  pale nyumbani kwake alipoamua kumuandalia wifi yake Masoi Sumayan sherehe ya kitchen party yaani , kwa kweli shughuli ilipendeza hasa pale unapowashirikisha wanawake wenzako, walikuwepo kama kawaida akina mama wa VG na majirani wengine wengi, mambo yalikuwa mambo, hebu twende tujionee kwa kiasi yaliyo jiri pale nyumbani kwa mama Sumayan.

MASOI SUMAYAN KITCHEN PARTY

 Masoi Sumayan siku ya kitchen part yake ilipendeza sana

 Wakina mama wa VG wakipongezana
Wakina mama wa VG wakiyarudi mangoma

Dada Eve akifungua chamapgne

 Ma MC wa shughuli hiyo wakibadilishana mawazo
 Ehh jirani sherehe imefana

















KWA MAMA SUMAYAN PALIKUWA HAPATOSHI

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa majirani na akina mama wa VG kuungana pamoja na kufurahia siku ya kitchen party ya Masoi Sumaiyan kwa kweli tulifurahi sana . Victoria au mama Sumaiyan alitokezea na vazi lake rasmi la huko kwao na alipendeza sana.

Wednesday, August 8, 2012

VG MAMA'S

VG  MAMA'S  SAFARI HII ILIKUWA KWA ROSE













Jumamosi tulikuwa nyumbani kwa Rose ,Maandalizi kwa dada huyu yalikuwa babu kubwa, kama ujuavyo mtu shughuli ikiwa kwako kukaa chini inakuwa nadra , mara umeitwa huku na kule ila mdada alijitaidi kubalance kwa kweli  tulikula tulikunjwa na tulifurahi , na mwisho bila kukosa tulishauriana na kuelimishana kama kawaida kwa akina mama  wanapokutana.

MAMA TENGENEZA JUICE NYUMBANI

SNACKS KWA WATOTO WA SHULE,
Mama Tengeneza Juice Nyumbani.

Leo naomba nizungumzie kuhusu snacks na vinjwaji  tunavyowafungia watoto wetu kwenda navyo shule,  Naomba sana  kwenu akina mama hebu mnapoandaa hizo snacks au juice mfikirie  hili . je ni muhimu sana mtoto wako aende na juice kila siku , hebu fikiria kumuwekea maji badala ya juice nasema hili kwa sababu watoto wengi wanapata usumbufu wa kuugua matumbo . mtoto wangu alikuwa na hili tatizo lakini nilipobadilisha chakula chake na kuanza kupaki maji na kuachana na juice na soda kweli amepona kabisa haugui tena tumbo na zaidi ya yote anapenda kunywa maji sana .

Wazazi tusipokuwa waangalifu watoto wetu watapata madhara hapo baadae, tuache uvivu tujishughulishe na watoto wetu zaidi kuchunguza wanachokula kila siku, hii ni pamoja na kuacha kuwapatia junk snacks na mengine mengi yanayofanana na hayo.

Kuna baadhi ya watoto wemekuwa na hili tatizo la kutokunywa maji , mimi naona ni tatizo kwani maji ni dawa, wewe mama hebu chunguza watoto wanakunjwa maji au akisikia kiu anaomba juice badala ya maji, ikiwa anafanya hivyo hebu chukuwa hatua ya kubadilisha hilo tatizo.

Juice nzuri ni ile amabayo wewe mama unaiandaa mwenyewe hapo nyumbani, juice ni nzuri kwa afya za watoto wetu, namaanisha juice ile wewe mama, au dada ameiandaa pale nyumbani, tuache uvivu tutumie matunda tuliyo nayo hapa nchini mwetu na tuandae juice zetu sisi nwenyewe, kuna misimu mingi ya matunda kwa hivi sasa kuna watermelons nyingi sana (matikiti maji) , machungwa yapo, embe ndio hizo zaja na mananasi halikadhalika, ukichunguza utakuta mwaka mzima tunamatunda ya kutosha hivyo ni jukumu lako wewe mama hebu chukuwa hatua tupunguze trip za mahosipitali kwa kubadilisha lishe zetu na watoto wetu.

Tuesday, August 7, 2012

Mpenzi wa blog hii, nimerudi tena,
Napenda chukua nafasi hii kukuomba radhi mpenzi wa blog hii kwani kutokana na mambo yaliyokuwa nje ya uwezo wangu nilikuwa sionekani bogini ila sasa nimerudi tena kuendelea kupeana ushauri na kuelimishana kama ukipata fursa ya kupitia blog hii.

MAZOEZI NI MUHIMU ?

sasa basi leo nimekuja na jambo moja muhimu kwetu sisi akina mama, kwamba hebu tutenge muda wa kufanya mazoezi kwani nimepitia vitabu mbalimbali na kuona kuwa maisha ya mwanadamu hasa kama unataka kuepukana na magonjwa au uzee ambao ungeweza ukauchelewesha  ni muhimu kufanya mazoezi.

utakubaliana na mimi kuwa maisha na ustaarabu wa maisha sasa umebadilika hasa , kama hapo awali ulikuwa unatumia daladala kwenda ofisini sasa unatumia gari, na ukifika ofisini badala ya kutumia ngazi unatumia lifti jamani haya ndio mabadiliko ambayo wengi wetu tunayapitia kila siku na mengine mengi yapo wewe unayajua.

sasa basi tufanye nini, kwa kusema hayo mimi naona zipo juhudi za makusudi inabidi kuzifanya ili tuweze kuishi miaka mingi, ili tuzitunze familia zetu na wale wanaotupenda. Jambo la muhimu la kufanya ni kufanya mazoezi pia kubadilisha ustaarabu wetu wa maisha kwa kubadisha hata jinsi tunavyooandaa vyakula vyetu  pamoja na kufanya mazoezi.

Changamoto wanazozipata wanawake wengi mimi nikiwa ni mmoja wapo ni kuamka asubui, kwa kweli nimezungumza na akina mama wengi na wamesema kuamka asubui ili kufanaya mazoezi ni vigumu sana kwao, pia ikizingatia kuwa wao pia ndio wanaowaandaa watoto kwenda shule na wale wasiotumia mabasi ya shule  inabidi mama wakati akielekea kazini kumpeleka mtoto shule ndio aendelee na shughuli zake. 

mimi nasema hiyo ni sababu tosha ya kukufanya usifanye mazoezi lakini sasa wataalamu wanasema  ni lazima ufanye mazoezi sasa uchaguzi ni wako . Bado ipo haja ya kufanya mazoezi kwani wewe mama ukisema huwezi kuna mama mwingine kama wewe yeye anaweza kitu cha msingi ni kupanga muda wako vizuri.

Friday, July 6, 2012

MTOTO MMOJA TU


NI KWELI WATOTO WAWILI TU?

Siku hizi kila mwanandoa utasiki anahitaji watoto wawili tu ni jambo zuri lakini unauhakika ni wawili tu, au ndio ile watoto wawili wa ndani ya ndoa na wengine nje ya ndoa. Mimi ni mmoja wapo wa wale wanaosema ni watoto wawili tu, lakini baada ya kufikiria na kuona mambo mengi nimegundua ni vizuri kuwa na watoto zaidi ya wawili.
Kwetu tumezaliwa watano na kimsingi, tumekuwa katika maisha ya kawaida sana na mungu ametujalia tumekwenda shule na sasa tunafanya kazi, tuna waangalia wazazi na familia zetu and life goes on . tunasaidiana pale mmoja wetu akikwama ila ni sisi tu tulizaliwa mama na baba mmoja, hakuna cha mtoto wa mjomba shangazi au baba mdogo ambaye anatoa msaada pale unapopata tatizo. Hivi ndivyo ilivyo kw siku hizi , tofauti na zamani enzi za mama zetu na baba zetu undugu ulikwenda zaidi ya ndugu mliozaliwa baba na mama mmoja. Yaani binamu zako wanakuwa sawa na kaka au dada uliyezaliwa nao.
Mimi baada ya kupitia mapito na kuona jinsi amabavyo undugu wa siku izi ulivyo yaani ni undugu wa kuzaliwa baba na mama mmoja ndio unaotambulika kwa sasa . nilirudi na kuiangalia familia yangu nikajiuliza je siku amabayo sitakuwepo hapa duniani na watoto wangu wawili wapo wenyewe itakuwaje?
Nikaangalia sisi tulio watano jinsi tunavyosaidina , kushauriana na n.k niliwaonea huruma watoto wangu wawili ndipo nikapata wazo la kuongeza mtoto lakini nikawa nimechele umri hauniruhusu sasa basi wewe ambaye Umri wako unakuruhusu hebu fikiria hili?

Hivi umeshawahi kumuona mama mwenye mtoto mmoja anavyohangaika yaani mtoto huyo ni kama mboni ya jicho, akiugua yeye ndio anaugua yaani anapata taabu mpaka utamuhurumia, hivyo kama mungu amekupa kizazi na unauwezo wa kumtunza mtoto ongeza mtoto mwingine isije kuwa majuto ni mjukuu. Kuna dada mmoja namnukuu alisema hivi

Husbands comes and go, money comes and go but the children they will be there with you forever

YES ALLOWANCE


Allowance Basics.
An allowance can be a great way to teach kids money management skills and help them learn how to make decisions, deal with limited resources, and understand the benefits of saving and charitable giving.
              There’s no single correct way to handle giving an allowance. Deciding when to start ,how much to give, and whether you want to link the allowance to chores are  that should fit your family.

Starting an Allowance.
No particular age is best for every kid, but  consider starting an allowance by the time  a child is 10 years old. By then ,most kids have had  experience  making thoughtful spending decisions  but still look to parents for guidance.
How much allowance  should you give? It depends on your financial situation and what kind of commitment you feel that you can comfortably keep. Experts generally recommend that kids get Tsh  500 Tsh to 1000 per week for every year of their age-Tsh 450 to 900 for 9yrs old ,for example
Regardless  of how much you choose, give the allowance regularly  and  increase the amount as your child gets older

Allowance and Chores.

Should an allowance be tied to chores? Again, it’s a personal choice. Some experts  think that it’s important to make this connection so that kids learn the relationship between work and pay. Others say    that kids should have a responsibility to help with housework, above and beyond any financial incentive.
Ultimately, you must decide  what works best for you. Whatever you decide, be sure that all parties understand the arrangement.
If you give an allowance for doing housework, make sure that your kids understand   what their responsibilities are and the  consequences of not doing them. You might want to involve them in choosing  the chores  and then keep a chart posted to remind them what needs to be done.
It’s  important to be consistent. Following through  on your promise to give a regular allowance sets a good example for your kids and is incentive for them to honor their end of  the bargain . If you don’t keep up with the allowance, they might lose that incentive and stop doing the chores.

Using an Allowance.

How should  kids spend their allowance? It’s good to have them use it for  discretionary things, not essential purchases such as food, clothing .This lets kids make buying decisions –and mistakes-without  dire consequences.
You might want to encourage  kids to put away a portion for charity and another portion for savings. If so, let them choose where to donate  the money. It  may be a cause that a child can relate to in  some way, like an animal shelter or a group that  helps sick  kids.
If  some of the allowance  goes to  savings, consider setting  up  an  account  at a local bank. This way, your  child   can keep track of the money. Many  banks offer special  bank accounts for  kids, and yours  may enjoy  the  experience of getting mail, even if the mail is a bank  statement.

Beyond Allowance.

Once kids become teenagers, you might want to provide a  quarterly clothing allowance  in addition to the weekly allowance.
If you do, establish a reasonable budget  and allow your kids to spend it as they wish – but also to honor its limits. If your son chooses  to buy a 9000  shirt and your daughter opts for a pricey handbag, for example, they might have to   make  compromises  on other clothing choices.

Monday, July 2, 2012

UMRI WA KUMTAIRI MTOTO

Ni Umri gani muhimu wa kumtairi mtoto wa kiume?

wazazi walio wengi huwa wanapata tabu kujua ni umri gani mzuri wa kumtairi mtoto, binafsi nilijaliwa kumtairi mtoto wangu akiwa na umri wa miezi miwili, japokuwa niliona nimewahi kumbe nilikuwa nimechelewa  , Wapo walio watairi watoto wao wakiwa na siku 7 yaani kama Yesu.

Ukiwa bado hujamtairi mtoto wako mama bado hujachelewa, kunafaida za kumtairi mtoto wako mapema. Kwanza kabisa unamuondolea maumivu makali kwani akitairiwa akiwa mkubwa huwa wanaumia sana. Faida nyingine ni ya kiafya zaidi umewahi sikia watoto wadogo wakisumbuliw na infections kwenye mkojo mara nyingi, utapunguza sana ugonjwa huu ikiwa utamtairi mtoto wako mapema. Zipo faida nyingi hivyo tutaendele tena kukuletea  topic hii.

Thursday, June 21, 2012

OFA BOMBA KUTOKA REX INVESTMENT


WAMAMA JE MWAJUA NJIA MBADALA ZA KUPATA UMEME,
Kuna kipindi hapa Tanzania tulipitia wakati mgumu wa kutokuwa na umeme, kutokana na mgawo ambao  ulisababishwa na kupungua kwa kiwango cha maji na mambo mengine mengi, Ndipo sa watu wakaanza kutafuta njia mbadala za kupata umeme ikiwa ni pamoja na Solar power, inventor ( Backup) na njingine nyingi. Ambazo zilipatikana kwa gharama kubwa.

Leo nimeona niongelee hili swala kwani nimegundua kuwa kuna watu wengi tuliumizwa na swala hili kwa kutugharimu kiasi kikubwa cha pesa kuliko ilivyo staili na ni kwa sababu ya kutokujua kinachoendelea huko madukani na wapi unaweza kupata kwa bei inayofaa na sio ya kuumiza sana.
Jana nilizungumza na rafiki yangu ambaye yeye anafanya kazi kwenye kampuni inayoshughulika na mambo haya ya umeme wa solar ameniambia mambo mengi na zaidi ya yote kilichonivutia zaidi ni Gharama zao.

Kwa kusema kweli nilishtushwa na gharama alizozisema kwani zilikuwa chini kiasi ambacho sikutegemea, kwani nilikuwa najua kuwa kuweka inventor ( Backup) inagharimu si chini ya 4m kumbe si kweli, zaidi ya yote akaniaambia pia Solar power wanayotoa ni cheap na genuine kwani zipo nyingine ni feki. Na unapogharamia ni mara moja tu halafu wewe unaendelea kutumia tu.
Hivyo basi akina mama wenzangu ili kuepukana na kero za kukatikiwa na umeme au kutokuwa na uhakika wa umeme mnaonaje mkafikiria kuweka solar. Kwani mara nyingi umeme ukikatika utakimbilia kuwasha mshumaa, sasa basi ili kuwasha tata za nje na ndani kwa solar unatakiwa uwe na kiasi si zaidi ya 1m. Kwa kiasi hicho utawasha taa za nje zote na ndani na ukiwa na wataalam wao wanauwezo wa kukuunganishai moja kwamoja  inakuwa kama standby generator yaani umeme ukikatika tu solar unaanza kazi yake.
Kwa kweli nawahamasisha wenzungu tujitahidi tuweke solar twende na wakati tupunguze ngarama na ajali zinazoweza sababishwa na mishumaa, hivyo kama utapenda anza kudunduliza sasa, ikifika 1m tu solar inapatikana kwako. Kama ujuaavyo nyumba ni mama umeme wa uhakika Tumia Solar.
Huduma hii inapatikana Rex Investment, wataalamu wa solar Power wenye uzoefu.Wahi kabla mgao haujaanza
Wanapatika hapa hapa Dar es saalam.

KWELI NI MTOTO ASIYEKUWA


KWELI MWANAUME NI MTOTO ASIYEKUWA,

Nakumbuka tulishawahi kuongelea kuwa mwanaume ni mtoto asiyekuwa na kwamba wewe mke wake ni sawa na mama yake, rafiki yake na pia ni mke wake. Mwanaume akiwa nyumbani tegemeo lake ni kwa mkewe hasa kwa kila kitu, vitu kama chakula, nguo, usafi utunzaji wa document hasa zinazowahusu hapo nyumbani, vyeti vyake, hati ya nyumba, n.k.
Wanachojua maadamu mama yupo hapo nyumbani yeye ndiye muangalizi wa kila kitu, ataitwa kwenye interview  atakuja atakuuliza wapi vyeti vyangu, mnataka mkopo wa nyumba atakuuliza wapi hati ya nyumba, mnataka lipa bili wapi bili za maji n.k hivyo wewe mama unatakiwa kuwa smart kwani wewe ndiye unayetunza document.

Sasa imefikia hatua mungu amewajalia mnakiwanja mnataka kujenga, hapo tena ni sehemu nyingine wanaume wanahitaji msukumo kutoka kwa wake zao, kwani nimeona na ninaona jinsi ambavyo wanawake wanavyo wasukuma waume zao kuanza ujenzi na kufanya shughuli za maendele kwa ujumla.
Si maanishai wanaume wote wapo wale amboa wakiamua fanya jambo hufanya bila kusukumwa au kukumbushwa na wapo wale ambao wewe mama ukinyamaza tu kama ni mkopo mliuchukua utashaa utapoambiwa umekwisha na mjengo hauja anza. Kimsingi kila mtu amuangalie mwenzi wake na kujua ni mtu wa aina gani? Si vibaya wewe mama ukianza halafu yeye akafuatia, ikiwa unafanya kazi na mnachokiwanja na kila ukimwambia mwenzio tuanze kujenga naye anakuwa kama anapotezea wewe sasa chukua hatua, kama unapesa nunu nondo, mchanga, na kokoto ukiweza nunua na matofali, nakumbia kasha mchukue mwenzi na uende naye huko kwenye site yenu, Kesho yake yeye mwenyewe atatafuta fundi na ujenzi utaanza. 
Imeshatokea hivyo, lengo langu leo ni kukuhimiza wewe mama kuchukua hatua ya kuanzisha jambo ambalo mwenzio bado analivutia pumzi.

KIDALI PO!


UNAKUMBUKA  MICHEZO YA UTOTONI?

Wazazi wenzungu mnakumbuka michezo ile ya zamani kabla hakujawa na TV, Computer, Play Stations n.k Tulikuwa tunacheza michezo gani.

Mimi nakumbuka, mnakumbuka mchezo unaitwa kidali, kombolela, ready na kadhalika, kwa kweli ilikuwa ni michezo mizuri sana na tulikuwa tunaifurahia sana. Hivi umeshajaribu kuwafundisha watoto wako hii michezo, japo kwa kuwaeleza tu kuwa hapo zamani ulikuwa unacheza michezo aina gani?. Mimi nafikiri ni wakati umefika wa kuwafundisha watoto wetu michezo yetu ya zamani, kwani kwanza licha ya kuwa ilikuwa inafurahisha pia ni mizuri kiafya.

Nimewakumbusha hili kwa sababu hivi sasa kuna tatizo kubwa kwa watoto wetu, ambalo ni la kukaa ndani muda mwingi na kutazama TV, video game, play stations n.k. Tatizo hili lina madhara kiafya kwani watoto wengi wameanza kulalamika, macho kuuma, migongo kuuma ,shingo n.k.

Sasa basi sisi wazazi inabidi tufanye juhudi za makusudi kwa kuwatafutia michezo tofauti ya  kucheza, Michezo ya kujificha, kombolela, yai bovu na mengine mingi inabidi irudi jamani na wa kuirudisha ni sisi wazazi tulio icheza kwa kuwafundisha watoto wetu, Mnakumbuka kuruka kamba  sikuizi kuruka kamba ni mpaka uende Gim.
Maendele ni mazuri lakini tusipokuwa waangalifu watoto wetu tunao wapenda watakuwa wameathirika na maendeleo haya .

Monday, June 18, 2012

CHARITY BEGINS AT HOME


Charity begins at home,

Mwezi huu ulikuwa na sherehe nyingi  moja wapo ilikuwa ni siku ya mazingira duniani, hapa Tanzania pia tullisherehekea sana, ila mimi napenda kuisherehekea kwa kukumbushana jinsi gani tunaweza kuifanya miji yetu kuwa safi, ila napenda usafi wa miji yetu uanzie majumbani mwetu.

Nimekwisha sikia kuna baadhi ya mikoa hapa Tanzania inaongoza kwa kuwa na mazingira safi moja ya mikoa hiyo ni Kilimanjaro hasa mji wa moshi, na mwingine ni Mwanza, jamani Tanzania yetu hii ni kubwa sna ila miji miwili tu ndio imeonekana kuwa safi kweli hebu tubadilikeni.

Kwa kuanzia majumbani mwetu kwa kuwafundisha watoto wetu usafi, wakiwa nyumbani hata pia wakiwa wapo nje ya majumba yao, hii ikiwa ni pamoja na unapokuwa barabarani, au sheleni, Kumfundisha mtoto kutotupa takataka mpaka akutane na mahali penye dust bin, mimi ninahakika tukifanya hivyo tutakuwa na kizazi kisafi hapo baadae na pia nchi safi. 

Saturday, June 16, 2012

FATHER'S DAY


Agness & Emmanuel sent this to their father ,

To dad  from your daughter,
I wear your shirts, your boots, your hat. A tomboy in a way, but I like that.
Comp or fishing, I’m just a mini you, We have so much fun whatever we do, Back in the woods or out by the water I will always love being your daughter.


To dad from your son
Who is my Father?
He made me,
Father is a source of strength, a teacher and guide, The one his family looks up to , with loving trust and pride, Father is a helper with a willing hand to lend, A partner and adviser, and the finest kind of friend.

Thursday, June 14, 2012

Cherrys Birthday is today












Cherry's Birthday is Today,

Asante mama for good present, i,m so luck that you are my Mother, today i.m seven years old, thanks god for the day, i,m so happy as you can see.

My Birthday

My Birthday,

 Look at lulu and lisa and Mesha
 Look at Naeema,Me, Ethan and Linda
Look at Adia,Nicole and Maya

 Hi Daniela,mesha and Glory
 Karungi and Rabia

Cath, Ansemol and Harry
 Kemi and Juanitha

My cousin Samwel
Naitwa Emmanuel, napenda kuwashukuru wanafunzi wenzangu wa kwanza International
School Grade 2, bila kumsahau Linda Lugalla Grade 1 kwa kusherehekea pamoja na mimi Birthday yangu , Napenda kuonyesha picha zenu hapa kwenye blog hii hebu ona.