Subscribe:

Ads 468x60px

Tuesday, June 12, 2012

MFUNDISHE MTOTO KURUDISHA KITU AMBACHO SI CHAKE


MFUNDISHE MTOTO KURUDISHA KITU AMBACHO SI CHAKE

Wazazi watoto wetu wanapokuwa mashuleni huwa wanachukuliana vitu vyao, mfano mtoto wangu siku moja alikuja na saa ya rafiki yake, nikamuuliza mbona una saa ambayo si yako, akasema nilimuomba rafiki yangu akanipa nivae, tena amesema ni yangu kabisa. Ukweli ni kwamba ilibidi nimwambie mtoto wangu amrudishie rafiki yake saa yake kwani saa ile si yake. Na pia nikamwambia wazazi wake watamuuliza saa yake iko wapi

Kwa mfano huo naomba wazazi  tushirikiane na walimu, kwani mara mtoto akipoteza kitu chochote, nafikiri kitu cha kwanza cha kufanya utamuuliza mwalimu wa darasa na ikitokea shuleni hutapata majibu ya kuridhisha utakuwa huna la kufanya. Kumbe ungemdadisi mtoto kwamba umempa nani saa, au kitu chochote kilichopotea angekwambia amepotezea wapi

Wazazi mtakubaliana na mimi mara nyingi watoto wetu wanapoteza vitu kama penseli, ruler, kichongeo na chupa za juice, folder na n.k . Utajikuta unanunua vitu hivyo mara kwa mara mpaka unachoka na katika hali ya kawaida hutaweza kumwacha mtoto aende shule bila kalamu au ruler hivyo utakuwa unanunua mara kwa mara. Hii ni changamoto  kwa mzazi na mwanae wa shule, ikiwa ni pamoja na kumuuliza mtoto na kumfundisha jinsi ya kutunza vitu vyake, na kumfundisha kukumbuka kuchukuwa kalamu au saa yake ikiwa amempa mwenzie au rafiki yake. Kingine cha msingi ni sisi wazazi kuwachunguza watoto wetu ikiwa wamekuja na vitu ambavyo si vyao na kumshauri kurudisha kwa rafiki au mwenzie aliye vichukuwa kwake.

Ili kwa kiasi kupunguza upotevu wa vitu vya shule kwa watoto wetu ni kufuatilia na kuwafundisha jinsi ya kutunza vitu vinavyowahusu, pia kumchunguza mwanao anapokuja na kitu ambacho si chake kumshauri akirudishe shuleni na kumpatia mwalimu. Kwani walimu huwa wanakuwa na taarifa za upoteaji wa vitu vya wanafunzi hivyo inakuwa rahisi pia kwao tukishirikiana nao kwa namna hiyo

No comments:

Post a Comment