Subscribe:

Ads 468x60px

Saturday, June 9, 2012

MWANANGU ANAKOJOA KITANDANI


MWANANGU ANAKOJOA KITANDANI , ANA MIAKA 12, NIFANYEJE,

Kitendo cha mtoto kukokoa kitandani akiwa na umri wa miaka zaidi ya kumi kweli si kitu cha kupuuza ni vizuri kutafuta njia za kumsaidia kuna njia amabzo mimi binafsi nimezitumia na zimenisaidia, na nilipowashirikisha baadhi ya marafiki zangu zimewasaidia,
Moja wapo ya njia hizo ni ushirikiano hapo nyumbani, kati ya mzazi na mtoto, unatakiwa kumshauri mtoto kutokula vitu vya majimaji masaa2 kabla hajaenda kulala, ikiwezekana anywe maji na vitu vingine kama soda au juice masaa 2 kabla hajakwenda kulala,
Pia anatakiwa kabla hajalala kuhakikisha hana mkojo ndani ya kibofu chake , namaanisha kwamba mtoto aende akakojoe kabla hajalala.
Pia ni vizuri usiku kuwe na mtu anakwenda kumwamsha ili aende akakojoe,lada ni dada au mtu yeyeto ukishtuka usiku labda unakwenda kujisaidia ni vizuri utumie wakati huo kumshtua naye aende kujisaidia.
Siku ikitokea kwa bahati mbaya amekojoa kitandani ni vizuri, kumuelewa, na kwa hakika atajisikia vizuri ikimuelewa, kwani hata yeye mtoto sidhani kama anapenda hali hiyo ya kujikojolea.
Kuna baadhi ya wazazi wanawapitisha watoto mitaani na kuwatangazia kuwa wanakojoa kitandani, au pia wanawatangazia kwa marafiki zao mashuleni au mtaani kweli hapo unakuwa ujamsaidia mtoto ila unamuaibisha tu.
Ukiangalia kwa undani hata mtoto mwenyewe hapendi kabisa, ila inakuwa ni hali tu imejitokeza hivyo ni vema kumsaidia na si vizuri kumuabisha kwani hali hiyo inamuumiza zaidi

1 comment:

Anonymous said...

Huyo sio kikojozi, mimi nina mtoto wa my sister ni kikojozi yaani nadhani ni doctor case, maana ana 5 yrs lkn akilala unaweza amshwa 6-7 times ndio hatakojoa, sasa inakuwa adhabu hata kwa yule aliye on duty wa kumwamsha, mtokeo yake anaachwa ajikojolee, mnaona ni bora kufua mashuka kuliko hiyo adhabu ya kumwamsha maana inakuwa almost wewe na mtoto mnakesha chooni..... nadhani hii ndio a kind of watoto vikojozi walivyo.. huo ushauri wako ni mzuri lakini ni 4 those wanaokojoa kibahati mbaya.

Post a Comment