Subscribe:

Ads 468x60px

Sunday, June 3, 2012

KITOVU CHA MTOTO, NA URIJALI?


KUNA UHUSIANO GANI KATI YA URIJALI NA KITOVU CHA MTOTO,

Nimesikia wazazi mbalimbali wakiongele swala la kitovu cha mtoto mchanga kudondokea kwenye uume wa mtoto kuwa unaleta madhara hapo baadae, Eti wanasema mtoto huyo ambaye kitovu chake kilidondokea kwenye uume wake atakuwa si rijali je kuna ukweli hapo?
Pia nimeona wazazi walimuwekea kidoti cheusi mtoto mchanga kwenye paji ati, kuzuia kwikwi inahusu vipi? Kumvalisha mtoto kitambaa chausi mkononi au kiunoni jamani inakuwaje, zaidi ya yote mtoto akiwa na kikoozi ambacho hakijapona kwa muda kidogo wanasema anakimeo?
Inakuwaje wewe mama umetoka kujifungua na unapelekwa kwa wazazi wako ati ukale uzazi kwa muda wa miezi 3, na huyo baba uliye zaa naye unamwacha ati hana uzoefu, kwani wewe unao, huoni kama unawasumbua wazazi wako, wakulee wewe na kisha wakulelee mwanao na zaidi ya yote ukae huko miezi zaidi ya 3 , sasa huyo baba mtoto atajua lini kulea mtoto mchanga, Baadhi ya watoto wachanga huwa wanalia sana usiku hivyo vilio huyo baba takuwa amevisikia saa ngapi kwake inakuwa ni adithi tu, mtoto ni wenu wote lakini kusota usiku kubembeleza mtoto usote mwenyewe na wazazi wako hebu fikiria. Kuna baadhi ya akina baba hawataki hata kuwashika watoto wao ati wanadai wanaona kama wanawaumiza jamani hutaki kushika mtoto wako mwenyewe?
Mimi ninaonelea hivi, mara mtu unapojifungua maadamu umeolewa na mumewako yupo hapo ni vizuri ukae hapohapo na usiende popote, mujifunze wote kwa pamoja kumlea mtoto wenu. Wewe mama unatakiwa ufanye juhudi za makusudi kumshirikisha mumeo sio unaambiwa tu nenda kwa mama ndio anajua na wewe unakubali, Ikiwa mtahitaji msaada wa kulea ni bora msaidizi huyo aje hapo kwako na akuelekeze nakisha aende. Zaidi ya yote madakitari wa watoto wapo kila kona hivyo usihofu kuwa jasiri.

No comments:

Post a Comment