Subscribe:

Ads 468x60px

Friday, June 1, 2012

ANAJUA KUSEMA ASANTE, KUSALIMIA JE?


MWANAO ANAJUA KUAMKIA NA KUSEMA ASANTE,

 Katika mila na desturi zetu watanzania tunatakiwa kuwafundisha watoto wetu tabia ambazo zinakubaliwa na jamii zinazotuzunguka. Moja ya tabia hizo ni tabia ya kusalimia, na kusema asante.
Kwa kweli usipomfundisha mtoto wako angali mdogo tabia hizi itakuwa ni vigume kuzifanya anapokuwa na umri mkubwa au hata kama atakuwa anasalimia ni mpaka akumbushwe. Hivi umeshawahi kutana na rafiki au jamaa na mtoto anakakataa kusalimia , unajisikiaje kweli inatia aibu mwenzenu yalinikuta .
Kwa kweli inapendeza sana mtoto anapokuwa na tabia nzuri, inapendeza pale unapompatia zawadi, au unapomfanyia kitu mtoto akasema asante, au nyie mwaonaje , Mimi imenisumbua sana kwa mtoto wangu alikuwa hawezi kumsalimia mtu bila kumwambia , mara nikutanapo na rafiki ,jamaa au ndugu kweli ilikuwa inani aibisha kwani ni mpaka aambiwe hujambo,  ndio naye atajibu sijambo, halafu inabidi umwambie tena sema shikamoo, ndi atasema shikamoo, kweli inatia aibu.
Sasa basi siku mmoja akaniuliza hivi mama how do you say shikamoo in English?
Kwa wenzetu wa ulaya wanapenda sana kusema sorry au, neon please, au kindly, au excuse me, haya ni maneno mazuri ya kuonyesha unyenyekevu na kujali mtu mwingine, mara nyingi mtumiaji wa maneno haya, anatumia pale ambapo anataka kufanya jambo au afanyiwe jambo, lakini anajua wazi kitu atakachokifanya kinaweza kisiwe kizuri kwa mtu mwingine, au kikamkwaza mtu mwingine, hivyo kwa kujali hali hiyo  na ndio maana atatumia maneno haya.
Kwetu sisi pia kuna baadhi ya  watu wanayatumia maneno haya pia pale tu anapozungumza kiingereza ila anapozungumza Kiswahili mara nyingine watu wanajisahau kutumia maneno kama haya ambayo ni, samahani, tafadhali, 

No comments:

Post a Comment