Subscribe:

Ads 468x60px

Sunday, September 30, 2012

MSAIDIZI WANGU MTU MZIMA


Msaidizi wangu ni mkubwa kuliko mimi ,


Wamama wenzangu nakuja kwenu na hoja hii nakomaje!!!!
Nina mama mtu mzima ambaye ananisaidia shughuli za hapa nyumbani sasa ni mwaka wa pili, watu wananisifu kuwa nimeweza kuishi naye muda mrefu kwani nikiwa kama bosi naonekana mdogo kuliko yeye kwani ana umbo kubwa na mungu kamjalia mashalaa.
Ukweli mpaka nimeona nifunguke humu ni kwamba nakuwa kama namuogopa ukweli ninamuogopa kwani kunabaadhi ya vitu nashidwa kumwambia ukizingatia kuwa mimi ndio mama mwenye nyumba. Sasa nimekuwa najiuliza nifanye nini ili niweze kurudisha umama wangu nyumbani kwangu.
Kabla sijawa na huyu dada nilikuwa na dada mwingine mdogo kiumri na pia alikuwa mdogo kiumbo tofauti na huyu niliye naye sasa. Ukweli nikilinganisha hapo awali nilikuwa naendana na dada huyu mdogo vizuri ikiwa kuelekezana hata akikosea niliweza kumgombeza kwamba mbona hapa hivi na pale vile. Sasa bwana kivumbi kipo hapa kwa huyu mtu mzima kwanza anajiona anajua na vilevile  akikosea kumwambia wewe nakomaje, naishia kufanya mwenyewe baadhi ya kazi zile ambazo huwa hazifanyi vizuri kwa kuhofia kumwambia pale anapokose.
Ukweli ni kwamba anafanya baadhi ya kazi vizuri, na baadhi anakosea ila kwa upande wake yeye anaona ni sawa, Kumuhitaji namuhitaji kwani sina mtu mwingine wa kunisaidia na vile unajua siku hizi kuwapata hawa akina dada ni kazi.
Nasikitika pale ninapoona nimekuwa dhaifu wa kumwambia anapokosea kwa vile namuogopa kwa vile yeye ni mkubwa na mimi ni mdogo, na pia naogopa akiondoka kwa sasa sina mtu mwingine na mimi ninafanya kazi za kuajiriwa. Najua wazi mimi ndio boss na ninamamlaka yote ila nashidwa kumkoromea. Nayeye naona ameshagundua udhaifu wangu huo ananiangalia tu nafikiri ananichora tu. Mume wangu ananishangaa na ameshawahi kuniambia mbona unamuogopa mfanyakazi wako kama amekushinda mwachishe kazi .
Marafiki zangu hawajui kero hii ya huyu dada, ila hawaishi kumsifia kuwa eeh msichana wako ni mchapa kazi kama nini, na wanataka wapate wamama watu wazimz kama mimi. Nisaidieni jamani nifanye nini?

No comments:

Post a Comment