Subscribe:

Ads 468x60px

Tuesday, March 20, 2012

Napenda kukushirikisha na wewe

Mama unayefanya kazi, umemuacha mtoto na dada nyumbani tangu asubuhi, hebu leo ukirudi umlishe mtoto wako chakula cha jioni wewe mwenyewe kama mama. kwani kutajenga mahusiano mazuri na mtoto wako.

Pia usisahau kuonja hicho chakula cha mtoto kwani ilikwisha tokea chakula cha mtoto kuwa na chumvi nyingi kupita kiasi . bila kuonja chakula hicho utasababisha mtot kuto kula vizuri.

Hebu pata muda kama mama au baba kuangalia hizo katuni ambazo mtoto wako ana angalia kwani wengi wetu tunaishia kuwaacha watoto wakiangalia katuni wenyewe bila kujua zina mauthui gani. kwani ilikwishatokea watoto kuangalia vitu vya kutisha na kuishia kuogopa kulala usiku.

wewe ni mama unayefanya kazi siku saba za wiki, huna muda wa kuwa na familia yako, kama mama lakini vipo vitu unaweza kufanya kwa ule muda mchache unaoupata, ukiwa nyumbani mtaweza kucheza karata, tengeneza pocorn, na mle pamoja kama familia, au siku ukiwa na muda wa kutosha mfanye window shopping.

kwa leo pata hizi dondoo chache, kwa ajili ya watoto


2 comments:

Anonymous said...

yap i like your profile it really remind us for things that mothers do take it easy but they are very important in rasing our children.As a mother even if your so bussy with work but make sure when you come back home cook for your kids, waogeshe, do homeworks together,give them foods by doing so u will realise new thins from them if the house assistant the never do to them.

Mama Melvin said...

nimeipenda sana hii topic, nilikuwa nagombana na mtoto wangu kuwa hali chakula dada yake anachompakia kwenda nacho shule. sasa siku moja akarudi na chips zake kutoka shule nikasema hebu nizile mimi wewe si unaringa! lol zile chips sikuweza kuzila chumvi mpaka ulimi unauma, ndio nikajua sababu. Tangu hapo lazima nionje kila kitu cha mtoto.

Post a Comment